Pages

Ads 468x60px

Featured Posts

Tuesday, April 29, 2014

FURSA: MAFUNZO YA KUPIGA ALA ZA MUZIKI KUANZA TENA MWEZI MEI‏

 Baadhi ya wanafunzi wakiwa kwenye mazoezi

Action Music Tanzania (AMTz) inatangaza fursa kwa watu wote kujiunga na mafunzo ya kupiga ala za muziki yanayoanza tarehe 3/5/2014, lengo likiwa ni kuwajengea uwezo wanamuziki wa kupiga ala na kufanya maonesho kwa weledi na utaalamu zaidi.
Baadhi ya wanafunzi wakiwa darasani

Mafunzo yanayotolewa ni pamoja na upigaji wa ala za muziki zikiwemo gita, kinanda, tarumbeta, saxophone, konga, drum set, na upigaji wa ngoma za asili. Pia yatatolewa mafunzo ya ‘body percussion’ yaani matumizi ya mwili katika kutengeneza midundo ya muziki.

Mafunzo hayo yanafanyika kwenye ofisi za AMTZ zilizopo maeneo ya Mwenge mtaa wa Umoja, nyuma ya magorofa ya jeshi na kwenye Idara ya Sanaa na Sanaa za Maonesho Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ambapo ili kujiunga na mafunzo haya wasiliana nao kwa simu namba 0686928828/0653075791 ili kupata fomu za kujiunga na mafunzo.


         


Sunday, October 27, 2013

Diamond Afunika Bukoba


IMG_0145
Ni Juma Nature, Mr Nice na Profesa Jay pekee waliowahi kufurahia mafanikio na kupendwa hivi anavyopendwa Diamond sasa.
Hitmaker huyo wa Kesho yupo ziarani mikoani na huko anapokelewa kama mfalme. March 30 alikuwa Bukoba mkoani Kagera na alikutana na mapokezi ambayo hawezi kusahau maishani.
Diamond akiwa amembeba shabiki mtoto
Diamond akiwa amembeba shabiki mtoto
Kupitia website yake Diamond ameandika:
Tarehe 30 March niliwasili salama salimini mjini Bukoba mkoani Kagera, pili niwashukuru mashabiki wangu wote mkoani kwa kunipokea kwa hali na mali. Hii inaonyesha jinsi gani watanzania wanathamini na wana mapenzi na wasanii wao. Nililazimika kutoka Juu ya Gari kuwasalimu kabla sijaelekea hotelini.
Nilivotokeza hali ilizidi kuwa mbaya zaidi. Polisi walilazimika kufunga barabara kadhaa mjini bukoba na hata kazi zingine kusimama kwa muda kutokana na watu kuzingira Gari nilokuwepo kila kona nilipokuwa pita.
IMG_0300
IMG_0317
Na katika show yake watu zaidi ya 3,000 waliingia na kusababisha mwandaaji kusitisha kuuza tiketi.
IMG_0093
IMG_0145
“Nilikinukisha vilivyo kama kawaida yangu na kuweka historia mpya ndani ya Bukoba kuwa mwanamuziki wa kwanza kupiga show mwenyewe na kujaza watu zaidi ya 3,000 hadi kufikia uongozi kusitisha kuuza ticket kutokana na jeshi la polisi kutoa taarifa ingeweza kutokea maafa kama ilivyotokea kabla ya mimi kupanda jukwaani.”